Jumanne , 1st Jun , 2021

'The vocalist master' Killy, ametumia zaidi ya siku 366 mpaka kutangaza ujio wake mpya baada ya kutoka Kings Music, lebo ya msanii Alikiba na kujiunga na Konde Music Worldwide lebo ya Harmonize, mapema mwezi Septemba 2020.

Msanii Killy

Harmonize ametangaza ujio wa mwimbaji huyo kupitia ukurasa wake wa instagram, huku akisema Juni 2, 2021 ni #KillyDay, akiwa na maana ndio tarehe rasmi ya Killy kuachia kazi yake tangu ajiunge na familia ya Konde Gang.

Inahisiwa kuwa huenda Killy akaachia album yake kwani Mei 3 mwaka huu, Harmonize alitudokeza kuwa album ya Killy imekamilika na tayari ana video 6 mkononi kutoka kwenye album hiyo.